Jumatano, 1 Juni 2016

UHUSIANO BAINA YA UNYAMBULISHAJI NA SINTAKSIA



Mchakato wowote unapofanyika huleta athari fulani kwenye tungo au neno linalohusika. Unyambulishaji ni moja ya mchakato ambao ukifanyika katika kitenzi unaleta athari katika vitenzi hivyo.        

 Na mchakato huu unaonesha uhusiano uliopo baina ya sintaksia na vitenzi vinavyonyambulishwa na visivyonyambulishwa. Hivyo, kuna baadhi ya vitenzi vikinyambulishwa vinachukua dhima moja na vingine vinachukua dhima mbili. Na kuna vitenzi  kwa asili yake havihitaji yambwa lakini unyambulishaji unavifanya vitenzi hivyo kuwa na sulubu dhima.   
          Uhusiano baina ya unyambulishaji na sintaksia unajitokeza katika mambo makuu matatu, kama ifuatavyo:
Kuongeza dhima                                                                                                                                Uongezaji dhima, utokea pale ambapo kitenzi ambacho hakina uwezo wa kubeba yambwa, hunyumbulishwa na kulazimishwa kubeba yambwa. Mchakato wa unyambulishi unakiwezesha kitenzi chenye sulubu dhima ya msingi kushiriki katika sulubu dhima nyingine na kwa kufanya hivyo huwezesha sentensi mbili kutungwa. Mfano:                                                                      
Ali amekufa (sulubu dhima moja)                                                                               tk
Ali amelif-i-a taifa lake (sulubu dhima mbili)                                                      td                                 tk
Katika mchakato huu wa kuongeza dhima au uongezaji dhima, kuna aina mbili za unyambulishaji zinazojitokeza nazo ni: unyambulishaji mufidi na unyambulishaji fanyizi.                            Unyambulishaji mufidi huu ni unyambulishaji wa uongezaji dhima kwa njia ya kupachika alomofo za kauli ya utendea yaani –e- na –i- katika kitenzi. Mfano:
       Swalo anapika (sulubu dhima moja)                                                                                                               tk        
        Swalo anampik-i-a mtoto (sulubu dhima mbili)                                                                                  td                    +fd    tk
       Stivin anasoma (sulubu dhima moja)                                                                                                           td
     Stivin anamsom-e-a Musa kitabu (sulubu dhima tatu)                                                                                       td                  +fd                 
           
Unyambulishi fanyizi, ni unyambulishi wa uongezaji dhima unaohusu upachikaji wa alomofu za kauli ya utendeshi katika kitenzi, alomofu hizo ni; -esh-, -ish-, na –z-. Mfano:
  Mtoto anaimba (sulubu dhima moja)                                                                                                  mtenda
 Mtoto anaimb-ish-a wimbo (sulubu dhima mbili)                                                                               mtenda                                    tk
Kupunguza dhima, uhusiano wa unyambulishi na sintaksia, pia hujidhihirisha katika upunguzaji dhima. Mchakato huu husababisha kauli tenda kubadilika na kuwa kauli tendeka baada ya kupachika alomofu za kauli ya kutendeka –k-, -ik- na –ek- na hivyo kitenzi chenye dhima ya utenda kupoteza dhima hiyo kutokana na unyambulishi tendeka. Mfano:
          Ali amemshik-i-a mwalimu kitabu (sulubu dhima tatu)                                                                      td                                 tk         tu
          Ali amekishik-il-a kitabu (sulubu dhima mbili)                                                                                   td                              tk
Hivyo, kitendo cha kubadili kauli tenda kwenda kauli tendeka kunachangia kuleta athari kubwa katika sintaksia kwani hupunguza dhima ya kitenzi katika sentensi.                                                            
   Kudhibiti dhima, hapa mchakato wa unyambulishi unapewa dhima mpya bila kubadili idadi ya dhima ndani ya sulubu dhima. Matokeo ya mchakato huu ni kwamba, kitenzi kinachatokea katika sulubu dhima na idadi ile ile ya nomino lakini dhima tofauti. Hapa kitenzi kipya hupata kauli tendwa na kuambikwa umbo la –w-. Mfano:
                   Swalo anapika chakula                                                                                   
                  Chakula kinapikwa na Swalo                                                                                                             
Mifano hiyo hapo juu, inaonesha kuwa sulubu dhima ni ileile, idadi  ya nomimo ni ileile, lakini tofauti ni ubadilishananji wa nafasi kati ya kiima na yambwa yaani sentensi ya pili, nafasi ya kiima imechukuliwa na yambwa na nafasi ya yambwa imechukuliwa na kiima.