SWALI:
Kwa
kutumia mifano, ainisha ngeli za nomino za Kiswahili, kwa kigezo cha
kimofolojia. Kisha jadili upungufu wa uainishaji huo.
Fasili ya ngeli
imejadiliwa na wataalamu na wanazuoni mbalimbali, huku kila mtaalamu akiwa na
mtazamo wake juu ya dhana hii. Baadhi ya wataalamu na wanazuoni hao ni kama
hawa wafuatayo:
Mgullu (1999: 148)
anasema istilahi “ngeli” imechukuliwa kutoka lugha ya Kihaya (Tanzania). Katika
lugha ya kihaya neno “ngeli” lina maana ya aina ya kitu.
Mgullu (1999: 148)
akiinukuu Kamusi ya Kiswahili Sanifu (1981) anaeleza kuwa ngeli ni utaratibu wa
taaluma ya sarufi ya lugha katika kupanga aina za majina (nomimo) kama vile
ki-vi, ma, n.k.
Mgullu anaendelea
kusema kuwa fasili hii inapotosha. Tuaamini ya kuwa ngeli ni kundi la nomino za
aina moja na si ule utaratibu wa kupanga nomino katika makundi kama fasili ya
hapo juu inavyodai.
TUKI (1990) wanaeleza
kuwa ngeli za nomino ni kundi moja la majina yaliyo na upatanisho wa kisarufi
unaofanana na viambishi vya umoja na wingi vinavyofanana. Fasili hii inaonekana
ni bora lakini tatizo lake ni kuwa imeweka pamoja vigezo viwili, yaani kigezo
cha kisintaksia na kile cha kimofolojia. Kwa maoni yangu ni kuwa vigezo hivi
haviwezi kutumika pamoja kwa sababu havina uhusiano wa moja kwa moja. Wanaisimu
na wachambuzi wengi wa awali walijaribu kuvitumia vigezo vyote viwili kwa
pamoja wakati wa kuainisha ngeli za nomino za Kiswahili lakini walishindwa.
Hali hii imesababisha uainishaji wa ngeli katika lugha ya Kiswahili uonekane
kuwa wa kutatanisha.
Massamba, D.P.B na
Wenzake (2012) wanasema kauli kwamba ngeli ni mgawanyiko wa aina mbalimbali za
nomino katika mtazamo wa kisarufi katika fikra ya viashirio vya nomino katika
aina nyingine za maneno zinazoandamana nazo. Kwa maelezo mafupi tunaweza kusema
ngeli za nomino huhusu makundi ya majina; kila kundi likiwa na mabadiliko ya
aina moja ya viambishi vya umoja na wingi vyenye kuleta upatanishi wa kisarufi
wa namna moja katika vitenzi, vivumishi na viwakilishi. Kila ngeli ina
kiambishi cha nomino zake ambacho kinatawala viambishi vinavyorejea nomino hiyo
katika aina hizo nyingine ziandamanazo nayo.
Massamba na Wenzake
wanaendelea kufafanua kuwa kila lugha inayotumia utaratibu wa ngeli huwa ina
idadi fulani ya ngeli. Si rahisi kusema kwa yakini hapo zamani lugha za kibantu
zilikuwa na ngeli ngapi, lakini tunajua kwamba kwa wastani lugha nyingi zina
ngeli zisizopungua kumi na zisizozidi ishirini.
Kwa ujumla, ngeli ni
aina au namna ya kupanga au kuweka majina katika makundi yanayofanana au
yanayowiana. Majina ya Kiswahili yanaweza kugawanywa katika makundi mbalimbali.
Baadhi ya wanaisimu wamegawanya majina katika makundi 16 na wengine katika
makundi 9 na wengine makundi 18. Wanaisimu tofauti walioainisha ngeli za majina
ya Kiswahili wamechunguza vipengele tofauti
vya majina na kuyaanisha tofauti. Nomino za lugha fulani zinaweza
kuainishwa kwa kutumia vigezo vikuu vitatu yaani:
·
Kigezo cha kisematiki
·
Kigezo cha kimofolojia
·
Kigezo cha kisintaksia
Lakini katika muktadha
huu tutajikita katika kujadili uainishaji wa ngeli za Kiswahili kwa kutumia
kigezo cha kimofolojia. Kigezo cha kimofolojia ni kigezo kikongwe zaidi
kilichotumiwa na wanasarufi mapokeo, miongoni mwao akiwa Meinhof ambao
waliyaainisha kulingana na maumbo ya viambishi awali vya majina. Majina yote
yalikuwa na viambishi awali vinavyofanana yaliwekwa katika kundi moja na
kufanya ngeli moja kutokana na kigezo hiki kuna ngeli 18 za Kiswahili.
Uainishaji wao ni kama ifuatavyo:
Ngeli
|
Mfano
wa majina ya Ngeli
|
1-Mu-
2-Wa-
|
Mzee
– wazee
Mtoto-
watoto
|
3-
M-
4-
Mi-
|
Mti
– miti
Mchungwa
– michungwa
|
5-
Ki-
6-
Vi-
|
Kiti-
viti
Kisu-
visu
|
7-
Ji-
8-
Ma-
|
Jiwe-
mawe
Jicho-
macho
|
9-
N-
10.
|
Nguo,
nchi, njaa, nyota, ngozi, nyama
|
11-
U-
12-
N-
|
Uso
– nyuso
Uzi
– nyuzi
Ulimi-
ndimi
|
13-
U-
14-
Ma-
|
Uasi
– maasi
Ugonjwa
– magonjwa
|
15-
Ku-
|
Kusoma
Kucheza
Kuimba
Kuruka
|
16-
Pa-
|
Pahali
|
17-
Mu-
|
Muhali
|
18-
Ku-
|
Kuhali
|
Wanaisimu wengine
Ashtoni (1944) na Broomfield (1930) waliainisha majina baada ya Meinhof,
walifuatisha mtindo wa Meinhof, isipokuwa wanayaweka katika ngeli moja majina
ya umoja na uwingi ambayo yanachangia mzizi mmoja badala ya kuyaona kuwa ni
tofauti. Kwa uainishaji huu walipunguza idadi ya ngeli hadi kufikia 9 tu.
Ngeli
|
Mifano
ya Majina
|
1-Mu/Wa
|
Mtoto
– watoto
Mpishi
– wapishi
Mchungaji
– wachungaji
Mkulima
– wakulima
Mtu
– watu
|
2-
M/Mi
|
Mti
– miti
Mwembe
– miembe
Mkono
– mikono
Mchoro
– michoro
|
3-
Ki/Vi
|
Kiti
– viti
Kitabu-
vitabu
Kito-vito
Kisu-visu
|
4-
N
|
Ngozi,
nyota, nyundo, njia, ngoma, njuga
|
5-
Ji/Ma
|
Jiwe
– mawe
Jino
– meno
|
6-
U/N
|
Uzi
– nyuzi
Uso
– nyuso
Ulimi
– ndimi
Ufa
– nyufa
|
7-U/Ma
|
Ugonjwa
– magonjwa
Uasi
– maasi
Ununuzi
– manunuzi
|
8-
Ku
|
Kuimba,
kucheza, kuoga, kupiga, kusoma, kuruka, kulima
|
9-
KU
PA
Mu
|
Mahali
Kule
Pale
Mule
|
Uainishaji wa akina
Ashton na Broomfield unafanana na ule wa Meinfoh kwa sababu wote wameegemea
uainishaji wao katika umbo la viambishi awali vya majina. Hata hivyo uainishaji
wao umekuwa mwepesi zaidi kwa mtu anayejifunza ngeli za majina kwa vile
unaonesha uhusiano wa umbo la umoja na uwingi la majina ya aina moja. Zaidi ya
hayo uchache wa ngeli hizi unamfanya mwanafunzi azikumbuke kwa urahisi.
Matatizo
(Mapungufu) ya kigezo hiki
-
Kuna viambishi ambavyo vinafanana,
mfano, ngeli ya kwanza inawakilishwa na kiambishi Mu, kiambishi hiki kinajitokeza vilevile katika ngeli ya pili na
ngeli ya tisa. Hali kadhalika vile vya ngeli ya nne na sita vinawakilishwa na
kiambishi N-, ngeli za sita na saba
inawakilishwa na kiambishi U-. kwa
ujumla hili ni tatizo.
-
Kuna majina mengine hayana umbo dhahiri
la umoja na uwingi mfano tunda, nguo. Hivyo inakuwa vigumu kuainisha majina
yasiyo na umbo dhahiri la umoja na uwingi kwa kutumia kigezo hiki.
-
Pia kigezo hiki kinachanganya majina ya
viumbe hai na visivyo viumbe hai mfano ngeli ya tatu Ki – Vi umoja uwingi
kiti viti (kiumbe kisicho na uhai) kijana vijana (kiumbe hai)
-
Kuna baadhi ya ngeli zina viambishi vya
umoja tu mfano ngeli ya nne inatumia kiambishi cha umoja N- .
-
Pia kigezo hiki hakitilii maanani muundo
wa sentensi.
Mgullu (1999: 156) naye
amejaribu kuainisha kwa kutumia kigezo hiki cha kimofolojia. Mgullu katika
kuhitimisha uainishaji wake anasema kuwa ngeli nomino za kimofolojia katika
lugha ya Kiswahili zipo tisa yaani ngeli za:
i.
MU-WA
ii.
M-MI
iii.
JI-MA
iv.
KI-VI
v.
U-N
vi.
U-MA
vii.
U-ϴ
viii.
ϴ-MA
ix.
ZISIZO NA KIAMBISHI (CHA IDADI) CHOCHOTE
Mgullu anaendelea
kufafanua kuwa katika uainishaji huu utagundua ya kuwa nomino zilizo na umoja
na wingi tumeweziweka katika kundi moja tu. Utaona ya kuwa uainishaji huu
unatuwezesha kuzigawa nomino zote za Kiswahili bila kuibakisha hata nomino
moja. Unaweza kufikiria nomino yoyote na utapata mahali muafaka unapoweza
kuiweka.
Dosari
za uainishaji wa Mgullu ni kuwa bado matatizo tulioyataja hapo juu kwa
wataalamu na wanaisimu wengine bado hata kwa Mgullu yamejitokeza sana mfano
kufanana kwa viambishi, baadhi ya ngeli hazina umoja na wingi, pia amechanganya
majina ya viumbe hai na visivyo hai na katika uainishaji wa Mgullu hatujaona
ngeli ya PA-MU-KU.
Hitimisho
Kwa kuwa tumeshaona mapungufu na matatizo ya
uainishaji wa wataalamu na wanaisimu hao, kuna haja ya wanaisimu na wanazuoni
kuendelea kufanya utafiti na uchunguzi ili kuondoa haya mapungufu.
VITABU
VYA REJEA
Massamba, D.P.B. na
Wenzake (1999). Sarufi Miundo ya
Kiswahili Sanifu (SAMIKISA) Sekondari
na Vyuo. Dar es Salaam: TUKI.
Mgullu, R.S. (1999). Mtalaa wa Isimu, Fonetiki, Fonolojia na
Mofolojia ya Kiswahili. Nairobi: Longhorn Publishers.
Rubanza, Y.I. (1996). Mofolojia ya Kiswahili. Dar es Salaam:
Chuo Kikuu cha Tanzania.
Taasisi ya Elimu
(1996). Kiswahili Kidato 1-4. Dar es
Salaam: Oxford University Press.
TUKI. (1981). Kamusi ya Kiswahili Sanifu. Dar es
Salaam: TUKI.
Swalo, D.B. (Muswada).
Darasa la Kiswahili: Kidato cha Tano na Sita
asanteni kazi nzuri
JibuFuta